Header Ads

Breaking News
recent

Ndembala akwea pipa kwenda sweden


Taarifa kutoka uongozi wa Simba zinaeleza kwamba, kiungo wao Said Hamisi ‘Ndemla’ safari yake ya kwenda nchini Sweden kufanya majaribio kwenye klabu ya AFC Eskilstuna imesogezwa mbele hadi Alhamisi November 9, 2017.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana, ilieleza Ndemla ataondoka leo jioni kuelekea Sweden kufanya majaribio ya siku 14 kwenye klabu ya AFC Eskilstuna  lakini hadi sasa hazitajwa sababu za mabadiliko hayo.
“Tunapenda kuwafahamisha kuwa  safari ya mchezaji wetu Hamis Said Juma Ndemla iliyokuwa ifanyike leo Jumanne imesogezwa mbele”-Haji Manara, Afisa Habari Simba.
“Ndemla ambaye amepata nafasi ya kwenda kufanya majaribio katika klabu ya AFC Eskilstuna inayoshiriki ligi kuu nchini Sweden ,sasa ataondoka nchini siku ya Alhamis ya tarehe 9 ya mwezi huu.”
“Mabadiliko haya ya safari hayataathiri muda wake wa majaribio katika klabu hiyo,ambapo atakuwa huko kwa siku 14.”

Hakuna maoni:

Inaendeshwa na Blogger.